Skip to main content
""Kwa msaaada zaidi wasiliana nasi kwa namba zifuatazo 0754031039/0655568468 AfyaLishe Tz kwa ajili yako""

COUNSELLING DESK

COUNSELLING DESK
Tumia huduma yetu ya ushauri, na kujadiliana. Kwa matatizo ya kifamilia, kibiashara, kielimu, kiafya, mahusiano na mfumo mzima wa maisha wasiliana nasi kwa 0754031039 au 0655568468

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA



UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA

Tumekua na tamaduni ya kuandaa uji wa lishe ya mtoto bila kufuata kanuni za uandaaji bora.

Madhara ya uji usio bora

📌Kusababisha magonjwa
📌Unenepaji usiofaa

Uandaaji bora wa uji lishe kwa mtoto


🏮Kitu cha msingi cha kuzingatia ni kuandaa uji utaoweza kumpatia mtoto virutubisho anavyohitaji kwa umri wake ili kusaidia ukuaji na maendeleo bora kwa afya ya mtoto.

📌Virutubisho muhimu zaidi kwa mtoto ni
🏮Wanga
Kuupa mwili nguvu
Mahindi/Mchele/Viazi n.k
🏮Protini
Hujenga mwili
Soya/Maharage n.k
🏮Mafuta
Kutia joto
Ufuta/Karanga n.k

Zingatia katika uandaaji

📌Tumia aina moja ya nafaka kwa kila kirutubishi.

🍲Kwanini?
Kila nafaka inakiwango chake cha uivaji, kutumia nafaka zaidi ya moja kwa ajili ya kupata kirutubishi husika ni hatari, maana: vinapo tofautiana kuiva kunaweza sababisha  maumivu ya tumbo na magonjwa mengine kwa mtoto.

📌 uwiano sahihi wa vyanzo vya nafaka.
Kwanini?
Kiwango cha virubishi anavyohitaji mtoto hutofautiana kulingana na mahitaji ya ukuaji na maendeleo ya mtoto

📌Uchanganyaji na uandaaji vyanzo virutubishe uwe katika hali ya usafi ili kuepuka magonjwa.


Uandaaji
🍲zingatia mahitaji

Formula ya mfano

🍲Mahitaji

🌽Mahindi ya njano - chanzo cha wanga
🌽Soya - chanzo cha protini
🌽Ufuta - chanzo cha mafuta

🍲Uwiano
🌽Chanzo cha Wanga kilo moja-1kg
🌽Chanzo cha Protini nusu kilo-1/2 kg
🌽Chanzo cha Mafuta  robo kilo-1/4 kg

🍲Uchanganyaji
🌽osha mahindi, soya, ufuta vizuri kila moja pekeake baada ya kuvichambua.

🌽Anika juani hakikisha vumbi halitaingia.

🌽Changanya vyanzo vyako na kisha saga.

🌽Unga tayari kwa matumizi.

MUHIMU

Uandaaji wa soya
🏮Ni muhimu kuhakikisha umetoa maganda ya soya vizuri maana katika ganda kuna aina ya kirutubishi kinachozuia unyonywaji wa kirutubisho cha protini katika mwili wa mtoto baada ya umeng'enyaji chakula.

Matumizi ya karanga
🏮 kama utatumia karanga katika usagaji, iandae na kuisaga peke yake na uichanganyie wakati wa kupika uji.

🍲Karanga huwai kuchacha joto likiongezeka ndio maana tunaiandaa pembeni na kuichanganyia wakati wa kupika ili kuweza kukinga kuchachisha na nafaka zingine ambapo kukitokea kutamletea madhara mtoto kama kuharisha.

🍲Karanga itumike ndani ya siku saba tu baada ya kusagwa maana baada ya hapo itakua imeshachacha.


🏮 Muda wa kupika uji
🍲Katika kupika uji wa mtoto hakikisha unapika uji kwa muda usiopungua nusu saa mpaka dakika 45 ili kuhakikisha kua umeiva vizuri.

🏮 kiwango cha virutubisho bora katika vaadhi ya nafaka
🍲Utumiaji wa mahindi ya njano au viazi vya njano kama chanzo cha wanga ni bora zaidi kwamaana vina kiwango kikubwa cha vitamini A, hii humsaidia mtoto katika :
🍲Kuimarisha macho yake

By Sylvia Senkoro
AfyaLishe Tz
0754031039/0655568468
sylsenkoro@gmail.com
afyalishetz@gmail.com

Comments

  1. Asante sana. Naomba kufahamu karanga ni bora kuzikaanga kabla ya kusaga?

    ReplyDelete
  2. Naomba nijue mwanangu bado hajatimiza miezi sita je atakapoa Anza tu Kula naweza kumuanzisha lishe moja kwa moja

    ReplyDelete
    Replies
    1. Unaweza kuanza lishe ila inatakiwa kuwa ni nyepesi na kidogo, unaanza kidogo kidogo hadi anazoea.

      Delete
    2. Tofauti ya soya na soya maziwa n nn? Na naruhusiwa kutumia soya maziwa?

      Delete
  3. Vipi mtoto wa miaka mitano soya yake naweza iacha na maganda?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hahaha ww kavivu kuandaa soya ee hahah

      Delete
    2. Zipo soya ambazo teali zimeshakobolewa yaani zimeshatolewa maganda na unapata kwenye maduka ya nafaka

      Delete
    3. Wapi hizo zapatikana mbona hatuzioni masokoni

      Delete
    4. Asante Sana Kwa elim nzuri nikitumia mbegu za maboga ktk mchanganyiko badala ya Karanga inafa na pia naruhudiwa kisaga pamoja au nayo nisage pembeni kama Karanga ulivyosema tusichanye mana huchacha

      Delete
  4. Ahsanten sana kwa elimu Nzur

    ReplyDelete
  5. Hii garage soya walitoa vipi maganda

    ReplyDelete
  6. Naomba kujua ni nafaka gani zinazotakiwa kukaangwa kabla ya kuzisaga tofauti na karanga?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Tushukuru sana kwa somo lenye maelekezo mazuri.
      Naomba kujua mtoto wa miezi sita anafaa kunywa uji wa lishe uliochanganywa na nafaka zaidi ya tatu?

      Delete
  7. Duh nimejifunza lkn hy soya jmn kuiandaa Ni kazi Lkn km unahtj mtt awe na lishe nzr Ni Bora kuiweka

    ReplyDelete
    Replies
    1. Na nikazi kweli huwa inachukua hata siku nzima ila kwa afya ya mtoto ni bora kuandaa tu

      Delete
  8. Ahsante kwa somo zuri..

    BARIKIWA

    ReplyDelete
  9. Asante sanaaz ila naomba kujuaa naweza kumuekea almond badala ya karanga

    ReplyDelete
  10. Nashkru kwa somo zuri Sana, barikiwa

    ReplyDelete
  11. Asanteee sana kumbe mm huwa nakosea namwekea mtt mavitu mengi mwili ata hauji raund hii nasaga kwa maelezo yako

    ReplyDelete
  12. Natamani kueleweshwa juu ya siku 1000 za mtoto

    ReplyDelete
  13. Naomba kuna ukikosa soya waweza tumia nn

    ReplyDelete
  14. Replies
    1. Mwanangu anapata choo kigumu nisaidiwe nifanyeje

      Delete
  15. Mbegu za maboga naweza tumia badala ya soya au husaidia nini kwenye lishe

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mnegu za maboga zina madini ya zinc kwa wingi kama n wa kiume basi hatakuja kupata shida ya nguvu za kiume

      Delete
  16. Na vipi ukitumia almond kama chanzo cha protein?

    ReplyDelete
  17. Je mtoto mwenye afya njema anatakiwa kudumu kwenye lishe ya uji kwa muda gani kabla ya kuingia lishe ya vyakula vya kupondaponda? Vipi kwa mtoto mwenye maradhi ya mara kwa mara au mtoto mwenye changamoto ya ulemavu hususani ulemavu wa viungo?

    ReplyDelete
  18. Asante sana kwa elimu hii nzuri kwa Jamii. Mungu akubariki sana.

    ReplyDelete

Post a Comment

NEWS

NEWS
Kula lishe bora kuepuka hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa.

Chagua afya leo.

EXCLUSIVE BREASTFEEDING

EXCLUSIVE BREASTFEEDING
Make sure your child gets breastfed exclussively for the first six months, the child shouod not be fed anything else not even water. This adds up to the child's immunity and increase chencea of proper development.

Popular posts from this blog

KANUNI BORA ZA KUMUANZISHIA MTOTO CHAKULA AFIKAPO MIEZI SITA

KANUNI BORA ZA KUMUANZISHIA MTOTO CHAKULA AFIKAPO MIEZI SITA 🏮 Kwanini nianze kumpa mtoto wa miezi 6 chakula kingine? 🍲Mtoto wa miezi sita ameanza kuwa na mahitaji ya virutubishi  kwa wingi zaidi ya anavyopata kutoka kwenye maziwa ya mama.

ONGEZA UWEZO WAKO WA KUMNYONYESHA MTOTO

ONGEZA UWEZO WAKO WA KUMNYONYESHA MTOTO Mtoto anyonye maziwa ya mama tu hadi ayakapotimiza Miezi sita. Utakua umemuepushia magonjwa na hatari zingine nyingi tu. Kama mama hana maziwa ya kutosha mtoto pia anaweza kupewa formula milk ila ni pale tu mama akiwa maefariki au akiwa na tatizo kama hilo la maziwa kuto tosha. Lakini ni muhimu mama kukazana kuhakikisha maziwa yanatosha ili mtoto awe katika hali salama na afya zaidi. Fahamu vitu vifuatavyo vimesaidia wengine 🍵Maziwa ya mama yametengenezwa na vtu vi3 vya muhimu *maji ambayo ndio mengi *Protein and *Fats 🍵 ni muhimu sana kufahamu kwamba  kutoka kwa  Maziwa kunahitaji activity ya hormones/ homoni ziwe stimulated, na kinachostimulate ni mtoto kunyonya au kuvuta chuchu Hivyo mtoto anavovuta au kunyonya chuchu ya mama yake ndivo hormones za kutengeneza  maziwa zinavozalishwa zaidi, hivyo kuleta matokeo chanya katika unyonyeshaji. Mama asikate tamaa kumueka mtoto kwenye chuchu hata kama maziwa hayatoki auni macha
""AHSANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU, KARIBU TENA/ THANK YOU FOR VISITING OUR BLOG, YOU ARE WELCOME""