Skip to main content
""Kwa msaaada zaidi wasiliana nasi kwa namba zifuatazo 0754031039/0655568468 AfyaLishe Tz kwa ajili yako""

COUNSELLING DESK

COUNSELLING DESK
Tumia huduma yetu ya ushauri, na kujadiliana. Kwa matatizo ya kifamilia, kibiashara, kielimu, kiafya, mahusiano na mfumo mzima wa maisha wasiliana nasi kwa 0754031039 au 0655568468

UANDAAJI MAZIWA YA SOYA UKIWA NYUMBANI


Maziwa ya Soya
Aina hii ni maarufu pia, na kwa kuwa yanatokana na mimea, maziwa haya hana cholesterol ( lehemu) - tofauti na maziwa ya kawaida. Maziwa ya Soya pia yana kiwango cha chini cha kalori kuliko maziwa ya ng'ombe, yana kalori takribani 130 kwa kila kikombe. Hakuna lactose  katika maziwa haya, aina ya protini inayoleta sana gesi tumboni, hivyo huyafanya kuwa mbadala muhimu kwa watu ambao wanakabiliwa na ugonjwa wa kushindwa kuvumilia lactose (lactose intolerance) katika mfumo wao wa umeng'enyaji, pamoja na watu wasiotumia bidhaa zitokanazo na wanyama pia (vegeterians) sababu haitoki kwa wanyama. 

Soya ni mboga nzuri sana, na maziwa yanayotokana na jamii hii yana utajiri wa potasiamu, protini na kalsiamu ikiwa mtengenezaji atayaimarisha na madini. Pia ni chanzo kikubwa cha vitamini A na vitamini B12, ambayo haipo katika aina nyingine za maziwa.
Maziwa ya Soya hutoa kiwango cha juu cha protini, pia ni bora kwa watu ambao wanajaribu kudhibiti uzito wao au kupunguza mafuta. Pia ina kiwango cha chini sana cha mafuta, ikilinganishwa na aina nyingine za maziwa. 

Moja ya masuala mabaya ya maziwa ya soya ni kwamba kunywa kwa wingi kunaweza kuwa na athari mbaya kwenye uzalishaji wako wa homoni, hivyo wale walio na matatizo ya tezi wanapaswa kuepuka kunywa maziwa haya, au kufanya hivyo tu na ruhusa ya daktari wao.

Jinsi ya kuandaa maziwa ya soya ukiwa nyumbani

Anza kwa kuichambua soya yako,  toa uchafu ioshe kisha iloweke kwenye maji kwa kipimo cha, vikombe viwili vya soya kwa maji lita moja, loweka soya yako kwa masaa 8.
Mwaga maji kisha toa maganda, hakikisha maganda yote yametoka. Maganda ya soya yana aina ya protini inayozuia aina zingine za protini kufyonzwa mwilini kama virutubisho hivyo tunayatoa kuepuka hili. Lakini si kwamba soya ina sumu kama ambavyo inafahamika na jamii kubwa.
Osha tena soya zako na maji safi
Anza kuweka kikombe kimoja cha soya kwenye blenda na maji safi na salama mililita 600 kisha saga hadi upate ulaini kaa juice au maziwa, rudia kusaga na soya zingine zilizobaki hivyo hivyo kwa kipimo hiko cha maji hadi soya zako ziishe.

Kisha mimina mchanganyiko wako kwenye sufuria safi na uchemshe mchaganyiko wako kwa moto wa kawaida hadi uchemke vizur, usikae mbali maana yanapanda juu kama maziwa ya ng'ombe, endelea kuchemsha kwa dakika angalau 20 huku ukikoroga.
Wakati unakoroga toa utando unaotokea juu kama ule wa maziwa ya ng'ombe tunza kwenye fridgr unaweza tumia kuungia mboga zako au chakula.
Zima jiko ukiona yameshachemka vizur, kisha chuja maziwa yako kwenye bakuli safi au jagi, tumoa chujio safi unaweza kuweka kitambaa kisafi cheupe juu ya chujio ili upate maziwa masafi zaidi
Unga unga utakaobaki unaweza pia kuutunza ukawa unaungia vyakula vyako, nao una virutubisho vingi hasa protini
Yaache maziwa yako yapoe kisha mimina kwenye kitunzio chako, labda ni chupa au glasi, unavyomimina unaweza tumia chujio pia ili kuhakikisha unapata maziwa masafi zaidi.
Maziwa yako yapo tayari kwa matumizi. Unaweza ukayanywa bila sukari au ukaweka sukari na ladha zozote unazohitaji ni wewe na matumizi yako.

By Resta Dietetics & Counselling 
0754031039
afyalishetz.blogspot.com

Karibu group letu la whatsapp:
LISHE BORA NA USHAURI
https://chat.whatsapp.com/BFXj5ZT2p794abU8NAxJ0k
Bonyeza link kujiunga.

Comments

  1. Habari,mie nimetengeneza kwanini yabakia kwenye chupa Kama uji? Na je Ni sawa kwa mtoto mdogo?

    ReplyDelete

Post a Comment

NEWS

NEWS
Kula lishe bora kuepuka hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa.

Chagua afya leo.

EXCLUSIVE BREASTFEEDING

EXCLUSIVE BREASTFEEDING
Make sure your child gets breastfed exclussively for the first six months, the child shouod not be fed anything else not even water. This adds up to the child's immunity and increase chencea of proper development.

Popular posts from this blog

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA Tumekua na tamaduni ya kuandaa uji wa lishe ya mtoto bila kufuata kanuni za uandaaji bora. Madhara ya uji usio bora

MORINGA BENEFITS/ FAIDA ZA MLONGE

MLONGE Inaweza kutumika kwa ajili ya upishi na dawa. Mbegu hizi ni chakula ila  zinapaswa kutafunwa, badala ya kuzimeza nzima nzima, pia ni muhimiu zikapikwa au kukaushwa kabla ya kuliwa, badala ya kula mbichi. UMUHIMU KATIKA LISHE Mbegu za Moringa ni chanzo kikubwa cha Madini chuma, Potasiamu, Vitamini A, Vitamini C, Calcium, Amino asidi, na Nyuzi za chakula/Fibers. FAIDA ZAKE KIUNDANI -Huongeza mfumo wa kinga ya mwili. -Hupunguza shinikizo la damu. -Kurahisisha upatikanaji wa usingizi, na -Kuongeza afya ya ngozi, nywele na mifupa. MAELEZO KWA KINA. Huongeza mfumo wa kinga ya mwili. Uchunguzi umegundua kwamba mbegu hizi zina tabia za kinga dhidi ya vimelea na virusi, kutokana na mkusanyiko wao mkubwa wa vitamini C, pamoja na viuasumu mbalimbali ambavyo kiujumla vinaimarisha kinga ya mwili. Kupungua uzito kwa sababu ya kiwango kikubwa cha nyuzi chakula/ Fiber, hizi zitasaidia kushibisha, na hivyo kupunguza tamaa ya kula isiyo rasmi. Msaada wa Kulala. R...
""AHSANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU, KARIBU TENA/ THANK YOU FOR VISITING OUR BLOG, YOU ARE WELCOME""