Skip to main content
""Kwa msaaada zaidi wasiliana nasi kwa namba zifuatazo 0754031039/0655568468 AfyaLishe Tz kwa ajili yako""

COUNSELLING DESK

COUNSELLING DESK
Tumia huduma yetu ya ushauri, na kujadiliana. Kwa matatizo ya kifamilia, kibiashara, kielimu, kiafya, mahusiano na mfumo mzima wa maisha wasiliana nasi kwa 0754031039 au 0655568468

KANUNI BORA ZA KUMUANZISHIA MTOTO CHAKULA AFIKAPO MIEZI SITA



KANUNI BORA ZA KUMUANZISHIA MTOTO CHAKULA AFIKAPO MIEZI SITA

🏮 Kwanini nianze kumpa mtoto wa miezi 6 chakula kingine?
🍲Mtoto wa miezi sita ameanza kuwa na mahitaji ya virutubishi  kwa wingi zaidi ya anavyopata kutoka kwenye maziwa ya mama.

🍲Mfumo wake wa mwili unaruhusu upokeaji.
🍲 Si rahisi kwake kupata allergy.


🏮Makosa tunayofanya katika kumuanzishia mtoto chakula afikapo miezi 6
🍲kumpa mtoto vyakula visivyo na virutubisho bora.
🍲kuwahi sana au kuchelewa sana kumuamzishia mtoto chakula kingine.
🍲mtoto kupewa chakula kodogo sana au mara chache sana na kupelekea kushindwa kutimiza mahitaji yake ya siku kwa ajili ya ukuaji.

🏮Muda gani bora kumuanzishia mtoto chakula?
🍲Mtoto anyonyeshwe tu maziwa ya mama tangu anazaliwa hadi afikishapo miezi sita bila kumpa hata maji, maziwa ya mama ni bora, yana kinga na yanatosha kumfikishia mtoto mahitaji yote ya lishe ya siku.
🍲Anapofikisha miezi sita, ndio mtoto aanze kupewa vyakula vingine, maana muda huu mfumo wake wa ukuaji na mahitaji yake huongezeka na maziwa ya mama pekee hayamtoshelezi, hivyo mtoto apewe chakula na kunyonyeshwa pia.

🏮Chakula kipi ni bora kumpa mtoto muda huu?
🍲 Vyenye virutubisho muhimu.
🍲Visivyo na viungo vingi.
🍲Rahisi kuliwa na mtoto.
🍲Vinavyopendelewa na mtoto.
🍲Vinavyopatikana kwa urahisi na unafuu.

🏮 Mfano wa vyakula sahihi mtoto kupewa.

🍲 Maziwa ya mama, huleta joto na virutubisho bora kwa kiasi kikubwa mpaka mtoto afikapo miezi 23.

🍲Nafaka hutia nguvu,  kumpa mtoto baadhi ya protini na vitamini, mfano; mchele, mtama, mahindi, mihogo, viazi

🍲Vitokanavyo na wanyama, huleta protini, madini na vitamini mfano; maini, nyama, samaki, mayai.

🍲Maziwa, huleta protini, nguvu, vitamini ,madini mfano;mtindi na maziwa

🍲 Mboga za majani na za rangi ya chungwa, huleta vitamini, mfano; spinach, karoti, maboga, viazi vitamu vya lishe.

🍲Jamii ya kunde, huleta protini kiasi, mfano;choroko, njegere, mharage

🍲Mafuta hutia joto, mfano; siagi

🍲Mbegu, huleta nguvu, mfano; siagi ya karanga, mbegu za maboga, tikiti.


🏮 Unamuanzishiaje mtoto lishe ya chakula kipya?
🍲Mpe mtoto chakula aina moja kisicho na viungo, kurahisisha upokeaji wake.
🍲Ruka siku saba na umuanzishie aina ingine ya chakula, kisicho na viungo.
🍲Mpe mtoto vijiko viwili mpaka vitatu vya chakula kipya kwa siku za mwanzo  ili kurahisisha upokeaji.
🍲Mtazame mtoto kwa ukaribu kupata matokeo baada ya kumpa chakula
Angalia vipele, kukohoa na kupiga chafya, au kuharisha. ni dalili za allergy.
🍲Pia  kurahisisha kujua tabia ya kula ya mtoto ( mvivu au mlaji kupitiliza)


🏮 Kanuni bora za lishe ya mtoto akiwa wa miezi sita hadi miaka miwili.
🍲Zingatia usafi  katika uandaaji na ulishaji.
🍲Usichanganye chakula kibichi na kilichopikwa wakati wa kuandaa, kulisha au kutunza.
🍲Ivisha vizuri
🍲Tunza chakula katika joto salama.
🍲Tumia maji safi na salama.
🍲Mlishe mtoto kwa upendo ukimuongelesha na kumhimiza kujitahidi kula.
🍲Zuia usumbufu katika mazingira yanayozunguka sehemu ya kumlishia mtoto.
Hii husaidia watoto ambao  ni wavivu kula.
🍲Ongeza kiasi cha chakula kidogo kidogo kadri mtoto akuavyo.
🍲Mlishe mtoto aina mbali mbali za vyakula kutimiza mahitaji muhimu ya virutubisho.
🍲Tumia virutubisho vilivyoandaliwa tayari kwa kitaalamu. Kulingana na mahitaji na upatikanaji.
🍲Kipindi mtoto aumwapo;

💉Ongeza kiasi cha vyakula vya kimiminika.

💉Mnyonyeshe zaidi na umhimize mtoto kwa upendo kula vyakula laini na apendavyo.

💉Mpe mtoto vyakula kiasi kiasi mara nyingi zaidi kumsaidia kuweza kula chakula cha kumtosha bila kuchoka.


🏮 Je ni kiasi gani cha chakula kinatosha kukamilisha mahitaji ya virutubisho kwa mtoto ?

🏮 Miezi 6
🍲uji laini au chakula kilichopondwa.
🍲Mtoto apewe milo 2 kwa siku.
🍲kwa kila mlo vijiko viwili mpaka vitatu vya chakula kwa siku pamoja na kunyonya maziwa ya mama.
🍲kama mtoto hanyonyi vya kutosha hakikisha anapata maziwa  yalioandaliwa vizuri kwa ujazo wa nusu lita kwa siku.

🏮 Miezi 7 hadi 8
🍲Mtoto apewe chakula kilicho pondwa au uji
🍲Ale mara 3 kwa siku
🍲Apewe sehemu mbili ya tatu kwenye kikombe chenye ujazo wa 250mls (robo lita)  kwa kila mlo.
🍲Aendelee kunyonya au maziwa yalioandaliwa nusu lita kwa siku.

🏮 Miezi 9 hadi 11
🍲vyakula vilivyopondwa au kukatwa vipande vidogo vidogo na ambavyo mtoto anaweza kuokota mwenyewe.
🍲apewe milo 3 kwa siku na mlo 1 wa kati.
🍲Apewe kiasi cha robo tatu ya kikombe chenye ujazo wa 250mls (robo lita) kila mlo.
🍲Aendelee kunyonya au maziwa yalioandaliwa nusu lita kwa siku.

🏮 Miezi 12 hadi  24
🍲Vyakula vya kawaida vya familia.
🍲vilivyopondwa au vilivyokatwa vipande kama vitahitajika mtoto apewe.
🍲Ale mara 3 kwa siku na milo ya kati mara 2.
🍲Apewe kiasi cha ujazo wa kikombe robo lita kwa kila mlo.



🏮 MUHIMU
🍲KUMPELEKA MTOTO CLINIKI KWA AJILI YA VIPIMO NA CHANJO KAMA UTAVYOELEKEZWA NA KITUO CHA AFYA KARIBU YAKO.
🍲MAJI SAFI NA SALAMA YA KUNYWA MTOTO APEWE KULINGANA NA ATAVYOHITAJI.

By Sylvia Senkoro
AfyaLishe tz
0754031039/0655568468
afyalishetz@gmail.com

Comments

  1. Nina jarida langu nimeliandaa linalo husu afya na chakula kwa mtoto je? Naweza shea nanyi?

    ReplyDelete
  2. Ikiwezekana andaa telgram group tujifunze vizuriiii

    ReplyDelete
  3. Kuna athari gani endapo moto anaanza uko kwa miezi 4 au 5?

    ReplyDelete
  4. Asante sana walau nimepata mwanga

    ReplyDelete

Post a Comment

NEWS

NEWS
Kula lishe bora kuepuka hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa.

Chagua afya leo.

EXCLUSIVE BREASTFEEDING

EXCLUSIVE BREASTFEEDING
Make sure your child gets breastfed exclussively for the first six months, the child shouod not be fed anything else not even water. This adds up to the child's immunity and increase chencea of proper development.

Popular posts from this blog

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA Tumekua na tamaduni ya kuandaa uji wa lishe ya mtoto bila kufuata kanuni za uandaaji bora. Madhara ya uji usio bora

ONGEZA UWEZO WAKO WA KUMNYONYESHA MTOTO

ONGEZA UWEZO WAKO WA KUMNYONYESHA MTOTO Mtoto anyonye maziwa ya mama tu hadi ayakapotimiza Miezi sita. Utakua umemuepushia magonjwa na hatari zingine nyingi tu. Kama mama hana maziwa ya kutosha mtoto pia anaweza kupewa formula milk ila ni pale tu mama akiwa maefariki au akiwa na tatizo kama hilo la maziwa kuto tosha. Lakini ni muhimu mama kukazana kuhakikisha maziwa yanatosha ili mtoto awe katika hali salama na afya zaidi. Fahamu vitu vifuatavyo vimesaidia wengine 🍵Maziwa ya mama yametengenezwa na vtu vi3 vya muhimu *maji ambayo ndio mengi *Protein and *Fats 🍵 ni muhimu sana kufahamu kwamba  kutoka kwa  Maziwa kunahitaji activity ya hormones/ homoni ziwe stimulated, na kinachostimulate ni mtoto kunyonya au kuvuta chuchu Hivyo mtoto anavovuta au kunyonya chuchu ya mama yake ndivo hormones za kutengeneza  maziwa zinavozalishwa zaidi, hivyo kuleta matokeo chanya katika unyonyeshaji. Mama asikate tamaa kumueka mtoto kwenye chuchu hata kama maziwa hayatoki auni macha
""AHSANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU, KARIBU TENA/ THANK YOU FOR VISITING OUR BLOG, YOU ARE WELCOME""