Skip to main content
""Kwa msaaada zaidi wasiliana nasi kwa namba zifuatazo 0754031039/0655568468 AfyaLishe Tz kwa ajili yako""

COUNSELLING DESK

COUNSELLING DESK
Tumia huduma yetu ya ushauri, na kujadiliana. Kwa matatizo ya kifamilia, kibiashara, kielimu, kiafya, mahusiano na mfumo mzima wa maisha wasiliana nasi kwa 0754031039 au 0655568468

UANDAAJI SAHIHI WA MAZIWA YA NG'OMBE KWA MTOTO MIEZI 6 HADI MWAKA.



UANDAAJI SAHIHI WA MAZIWA YA NG'OMBE KWA MTOTO MIEZI 6 HADI MWAKA.
🏮Mfumo wa kumeng'enya chakula kwa mtoto wa miezi 6 hadi mwaka bado haupo na uwezo wa kumengenya virutubisho vilivyopo kwenye maziwa ya ng'ombe

🏮usipoyataarisha maziwa hayo inavyotakiwa kabla ya kumpa mtoto unaweza kumsababishia;

🍼maumivu ya tumbo sababu ya kujaa gesi (kiwango kikubwa cha casein aina ya protini zilizopo kwenye maziwa ya ng'ombe )

🍼chembe za kupata allergy kutokana na (whey) aina za protini zilizopo kwenye maziwa hayo ambavyo uwiano wake ni mkubwa kuzidi uwezo wa umeng'enyaji chakula kwa mtoto.

🍼🍼🍼🍼🍼🍼🍼
Jinsi ya kutayarisha maziwa ya ng'ombe kwa kumpa mtoto (miezi 6 hadi mwaka)

🏮 Mahitaji
Maziwa ya ng'ombe
Maji salama
Sukari

🏮 Uwiano
Ili kupata 400mls za mchanganyiko.

🍼Maziwa ya ng'ombe- Robo lita 250mls

🍼Maji salama- Nusu ya robo 125 mls

🍼Sukari -  vijiko 2 na nusu vya chakula 25g

 🏮 Upikaji
🍼Changanya mchanganyiko wako kwa uwiano hapo juu.
🍼Chemsha mchanganyiko huo, hakikisha maziwa yameiva.

🏮 Kiasi cha kupewa mtoto
🍼Mtoto apewe mls 500 kwa siku pamoja na chakula kingine.

By Sylvia Senkoro
AfyaLishe Tz
Contacts: 0754031039/0655568468
sylsenkoro@gmail.com
afyalishetz@gmail.com

Comments

  1. Asante sana Mtaalamu wetu Sylvia Senkoro wengi hautjui hili la uchanganyaji wa maziwa ya ngombe kwaajili ya kumuandalia mtoto wa anaeanza kula

    ReplyDelete
  2. Ahsante sana madam, je kuna ulazima wa kuweka sukar?

    ReplyDelete
  3. Thank you sanaaaa mwanangu kwenye kula anasumbua sana hivyo nilikuwa nafikiria jinsi ya kumpa maziwa ya ng'ombe..Nashukuru kwa somo.

    ReplyDelete

Post a Comment

NEWS

NEWS
Kula lishe bora kuepuka hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa.

Chagua afya leo.

EXCLUSIVE BREASTFEEDING

EXCLUSIVE BREASTFEEDING
Make sure your child gets breastfed exclussively for the first six months, the child shouod not be fed anything else not even water. This adds up to the child's immunity and increase chencea of proper development.

Popular posts from this blog

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA Tumekua na tamaduni ya kuandaa uji wa lishe ya mtoto bila kufuata kanuni za uandaaji bora. Madhara ya uji usio bora

UANDAAJI MAZIWA YA SOYA UKIWA NYUMBANI

Maziwa ya Soya Aina hii ni maarufu pia, na kwa kuwa yanatokana na mimea, maziwa haya hana cholesterol ( lehemu) - tofauti na maziwa ya kawaida. Maziwa ya Soya pia yana kiwango cha chini cha kalori kuliko maziwa ya ng'ombe, yana kalori takribani 130 kwa kila kikombe. Hakuna lactose  katika maziwa haya, aina ya protini inayoleta sana gesi tumboni, hivyo huyafanya kuwa mbadala muhimu kwa watu ambao wanakabiliwa na ugonjwa wa kushindwa kuvumilia lactose (lactose intolerance) katika mfumo wao wa umeng'enyaji, pamoja na watu wasiotumia bidhaa zitokanazo na wanyama pia (vegeterians) sababu haitoki kwa wanyama.  Soya ni mboga nzuri sana, na maziwa yanayotokana na jamii hii yana utajiri wa potasiamu, protini na kalsiamu ikiwa mtengenezaji atayaimarisha na madini. Pia ni chanzo kikubwa cha vitamini A na vitamini B12, ambayo haipo katika aina nyingine za maziwa. Maziwa ya Soya hutoa kiwango cha juu cha protini, pia ni bora kwa watu ambao wanajaribu kudhibiti uzito wao au kupu...

MORINGA BENEFITS/ FAIDA ZA MLONGE

MLONGE Inaweza kutumika kwa ajili ya upishi na dawa. Mbegu hizi ni chakula ila  zinapaswa kutafunwa, badala ya kuzimeza nzima nzima, pia ni muhimiu zikapikwa au kukaushwa kabla ya kuliwa, badala ya kula mbichi. UMUHIMU KATIKA LISHE Mbegu za Moringa ni chanzo kikubwa cha Madini chuma, Potasiamu, Vitamini A, Vitamini C, Calcium, Amino asidi, na Nyuzi za chakula/Fibers. FAIDA ZAKE KIUNDANI -Huongeza mfumo wa kinga ya mwili. -Hupunguza shinikizo la damu. -Kurahisisha upatikanaji wa usingizi, na -Kuongeza afya ya ngozi, nywele na mifupa. MAELEZO KWA KINA. Huongeza mfumo wa kinga ya mwili. Uchunguzi umegundua kwamba mbegu hizi zina tabia za kinga dhidi ya vimelea na virusi, kutokana na mkusanyiko wao mkubwa wa vitamini C, pamoja na viuasumu mbalimbali ambavyo kiujumla vinaimarisha kinga ya mwili. Kupungua uzito kwa sababu ya kiwango kikubwa cha nyuzi chakula/ Fiber, hizi zitasaidia kushibisha, na hivyo kupunguza tamaa ya kula isiyo rasmi. Msaada wa Kulala. R...
""AHSANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU, KARIBU TENA/ THANK YOU FOR VISITING OUR BLOG, YOU ARE WELCOME""