Skip to main content
""Kwa msaaada zaidi wasiliana nasi kwa namba zifuatazo 0754031039/0655568468 AfyaLishe Tz kwa ajili yako""

COUNSELLING DESK

COUNSELLING DESK
Tumia huduma yetu ya ushauri, na kujadiliana. Kwa matatizo ya kifamilia, kibiashara, kielimu, kiafya, mahusiano na mfumo mzima wa maisha wasiliana nasi kwa 0754031039 au 0655568468

UANDAAJI SAHIHI WA MAZIWA YA NG'OMBE KWA MTOTO MIEZI 6 HADI MWAKA.



UANDAAJI SAHIHI WA MAZIWA YA NG'OMBE KWA MTOTO MIEZI 6 HADI MWAKA.
🏮Mfumo wa kumeng'enya chakula kwa mtoto wa miezi 6 hadi mwaka bado haupo na uwezo wa kumengenya virutubisho vilivyopo kwenye maziwa ya ng'ombe

🏮usipoyataarisha maziwa hayo inavyotakiwa kabla ya kumpa mtoto unaweza kumsababishia;

🍼maumivu ya tumbo sababu ya kujaa gesi (kiwango kikubwa cha casein aina ya protini zilizopo kwenye maziwa ya ng'ombe )

🍼chembe za kupata allergy kutokana na (whey) aina za protini zilizopo kwenye maziwa hayo ambavyo uwiano wake ni mkubwa kuzidi uwezo wa umeng'enyaji chakula kwa mtoto.

🍼🍼🍼🍼🍼🍼🍼
Jinsi ya kutayarisha maziwa ya ng'ombe kwa kumpa mtoto (miezi 6 hadi mwaka)

🏮 Mahitaji
Maziwa ya ng'ombe
Maji salama
Sukari

🏮 Uwiano
Ili kupata 400mls za mchanganyiko.

🍼Maziwa ya ng'ombe- Robo lita 250mls

🍼Maji salama- Nusu ya robo 125 mls

🍼Sukari -  vijiko 2 na nusu vya chakula 25g

 🏮 Upikaji
🍼Changanya mchanganyiko wako kwa uwiano hapo juu.
🍼Chemsha mchanganyiko huo, hakikisha maziwa yameiva.

🏮 Kiasi cha kupewa mtoto
🍼Mtoto apewe mls 500 kwa siku pamoja na chakula kingine.

By Sylvia Senkoro
AfyaLishe Tz
Contacts: 0754031039/0655568468
sylsenkoro@gmail.com
afyalishetz@gmail.com

Comments

  1. Asante sana Mtaalamu wetu Sylvia Senkoro wengi hautjui hili la uchanganyaji wa maziwa ya ngombe kwaajili ya kumuandalia mtoto wa anaeanza kula

    ReplyDelete
  2. Ahsante sana madam, je kuna ulazima wa kuweka sukar?

    ReplyDelete
  3. Thank you sanaaaa mwanangu kwenye kula anasumbua sana hivyo nilikuwa nafikiria jinsi ya kumpa maziwa ya ng'ombe..Nashukuru kwa somo.

    ReplyDelete

Post a Comment

NEWS

NEWS
Kula lishe bora kuepuka hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa.

Chagua afya leo.

EXCLUSIVE BREASTFEEDING

EXCLUSIVE BREASTFEEDING
Make sure your child gets breastfed exclussively for the first six months, the child shouod not be fed anything else not even water. This adds up to the child's immunity and increase chencea of proper development.

Popular posts from this blog

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA Tumekua na tamaduni ya kuandaa uji wa lishe ya mtoto bila kufuata kanuni za uandaaji bora. Madhara ya uji usio bora

KANUNI BORA ZA KUMUANZISHIA MTOTO CHAKULA AFIKAPO MIEZI SITA

KANUNI BORA ZA KUMUANZISHIA MTOTO CHAKULA AFIKAPO MIEZI SITA 🏮 Kwanini nianze kumpa mtoto wa miezi 6 chakula kingine? 🍲Mtoto wa miezi sita ameanza kuwa na mahitaji ya virutubishi  kwa wingi zaidi ya anavyopata kutoka kwenye maziwa ya mama.

ONGEZA UWEZO WAKO WA KUMNYONYESHA MTOTO

ONGEZA UWEZO WAKO WA KUMNYONYESHA MTOTO Mtoto anyonye maziwa ya mama tu hadi ayakapotimiza Miezi sita. Utakua umemuepushia magonjwa na hatari zingine nyingi tu. Kama mama hana maziwa ya kutosha mtoto pia anaweza kupewa formula milk ila ni pale tu mama akiwa maefariki au akiwa na tatizo kama hilo la maziwa kuto tosha. Lakini ni muhimu mama kukazana kuhakikisha maziwa yanatosha ili mtoto awe katika hali salama na afya zaidi. Fahamu vitu vifuatavyo vimesaidia wengine 🍵Maziwa ya mama yametengenezwa na vtu vi3 vya muhimu *maji ambayo ndio mengi *Protein and *Fats 🍵 ni muhimu sana kufahamu kwamba  kutoka kwa  Maziwa kunahitaji activity ya hormones/ homoni ziwe stimulated, na kinachostimulate ni mtoto kunyonya au kuvuta chuchu Hivyo mtoto anavovuta au kunyonya chuchu ya mama yake ndivo hormones za kutengeneza  maziwa zinavozalishwa zaidi, hivyo kuleta matokeo chanya katika unyonyeshaji. Mama asikate tamaa kumueka mtoto kwenye chuchu hata kama maziwa hayatoki auni macha
""AHSANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU, KARIBU TENA/ THANK YOU FOR VISITING OUR BLOG, YOU ARE WELCOME""