Skip to main content
""Kwa msaaada zaidi wasiliana nasi kwa namba zifuatazo 0754031039/0655568468 AfyaLishe Tz kwa ajili yako""

COUNSELLING DESK

COUNSELLING DESK
Tumia huduma yetu ya ushauri, na kujadiliana. Kwa matatizo ya kifamilia, kibiashara, kielimu, kiafya, mahusiano na mfumo mzima wa maisha wasiliana nasi kwa 0754031039 au 0655568468

BAADHI YA VITU VYA KUZINGATIA TUNAVOUKARIBISHA MWEZI MPYA, WIKI MPYA NA SIKU MPYA.


```●Nina furaha kukwaambia kwamba bado hujachelewa kuweka lengo jipya na kuamua kulifanyia kazi katika safari inayoendelea katika maishs yako.

●Zifuatazo ni baadhi ya mifumo ya maisha inayoweza kukufanya ufanikishe malengo yako muhimu katika maisha.```

1. Ona kushindwa kama mwanzo wa kitu kipya

2. Mshirikishe Mungu kabla ya jambo lolote

3. Andaa nguo nadhifu ya kuvaa kesho kabla hujalala, amka mapema, tandika kitanda chako na  usisahau kujali afya yako.

4. Tafuta amani na yaliyopita kabla hayajakutesa

5. Weka malengo makubwa lakini anza na dogo lililo ndani ya  uwezo wako

6. Usiwekee labda katika vitu bali pima kilakitu

7. Usijifananishe na watu

8. Andika malengo yako

9. Panga mipango ya namna utatimiza malengo yako

10. Tafuta hekima na maarifa juu ya mambo mbali mbali hasa lile unslotazamia kufanya.

11. Fanya kazi yenye manufaa kwako

12. Tumia kidogo zaidi ya unacho ingiza

13. Wekeza katika mawazo yako

14. Kopa kwa manufaa

15. Epuka wapoteza muda

16. Tunza mahusiano yenye manufaa

17. Kutana na watu wapya waliokuzidi hatua fulani ya kimaendeleo.

18. Ni vizuri kuwafahamu wakosoaji wako na fahamu wanachokosoa na ukifanyie kazi kama kina mantiki.

19. Baki katika muelekeo wako

20. Chukua hatua baada ya kupima manufaa

21. Jifunze kwa unaowatamani

22. Chukua hatua hata kama inaogopesha

23. Tafuta maana yenye kutia moyo katika jambo umalofanya

24. Fanya kitu kimoja kwa wakati.

25. Kifanye taratibu kwa ufanisi na kwa ufasaha.

26. Fanya zaid ya unavyotegemewa

27. Kuwa mtu wa watu na Fundisha watu unachojua

28. Tengeneza tabia ya kuwa wa kushukuru

29. Weka muda wa kuwa karibu na familia yako na kuwasikiliza

30. Usitafute maisha ukasahau kuishi, pumzika na jiburudishe kwa kiasi.


```●Kumbuka mawazo hasi au mawazo ya changamoto unazopitia hayana budi kuja ila ni wewe utakaeamua jinsi yatakavyotengeneza au haribu maisha yako.

●Nashauri kuwa na mtu wa karibu atakae kusaidia kubeba yako ya moyoni na kukutia moyo katika kila jambo, ni muhimu pia kuwa na mtaalamu wa ushauri (counselling specialist).```

Nashukuru kwa kupitia makala hii. Usisahau kusubscribe blog yangu ili uwe wa kwanza kupata mambo mapya kila siku.

By Resta Dietetics and Counselling
0754031039

```Karibu kwenye group letu, ujifunze lishe bora na mambo mengine mengi.```

https://chat.whatsapp.com/BFXj5ZT2p794abU8NAxJ0k


```Bonyeza link hapo juu kujiunga moja kwa moja.```

Comments

NEWS

NEWS
Kula lishe bora kuepuka hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa.

Chagua afya leo.

EXCLUSIVE BREASTFEEDING

EXCLUSIVE BREASTFEEDING
Make sure your child gets breastfed exclussively for the first six months, the child shouod not be fed anything else not even water. This adds up to the child's immunity and increase chencea of proper development.

Popular posts from this blog

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA Tumekua na tamaduni ya kuandaa uji wa lishe ya mtoto bila kufuata kanuni za uandaaji bora. Madhara ya uji usio bora

UANDAAJI MAZIWA YA SOYA UKIWA NYUMBANI

Maziwa ya Soya Aina hii ni maarufu pia, na kwa kuwa yanatokana na mimea, maziwa haya hana cholesterol ( lehemu) - tofauti na maziwa ya kawaida. Maziwa ya Soya pia yana kiwango cha chini cha kalori kuliko maziwa ya ng'ombe, yana kalori takribani 130 kwa kila kikombe. Hakuna lactose  katika maziwa haya, aina ya protini inayoleta sana gesi tumboni, hivyo huyafanya kuwa mbadala muhimu kwa watu ambao wanakabiliwa na ugonjwa wa kushindwa kuvumilia lactose (lactose intolerance) katika mfumo wao wa umeng'enyaji, pamoja na watu wasiotumia bidhaa zitokanazo na wanyama pia (vegeterians) sababu haitoki kwa wanyama.  Soya ni mboga nzuri sana, na maziwa yanayotokana na jamii hii yana utajiri wa potasiamu, protini na kalsiamu ikiwa mtengenezaji atayaimarisha na madini. Pia ni chanzo kikubwa cha vitamini A na vitamini B12, ambayo haipo katika aina nyingine za maziwa. Maziwa ya Soya hutoa kiwango cha juu cha protini, pia ni bora kwa watu ambao wanajaribu kudhibiti uzito wao au kupu...

MORINGA BENEFITS/ FAIDA ZA MLONGE

MLONGE Inaweza kutumika kwa ajili ya upishi na dawa. Mbegu hizi ni chakula ila  zinapaswa kutafunwa, badala ya kuzimeza nzima nzima, pia ni muhimiu zikapikwa au kukaushwa kabla ya kuliwa, badala ya kula mbichi. UMUHIMU KATIKA LISHE Mbegu za Moringa ni chanzo kikubwa cha Madini chuma, Potasiamu, Vitamini A, Vitamini C, Calcium, Amino asidi, na Nyuzi za chakula/Fibers. FAIDA ZAKE KIUNDANI -Huongeza mfumo wa kinga ya mwili. -Hupunguza shinikizo la damu. -Kurahisisha upatikanaji wa usingizi, na -Kuongeza afya ya ngozi, nywele na mifupa. MAELEZO KWA KINA. Huongeza mfumo wa kinga ya mwili. Uchunguzi umegundua kwamba mbegu hizi zina tabia za kinga dhidi ya vimelea na virusi, kutokana na mkusanyiko wao mkubwa wa vitamini C, pamoja na viuasumu mbalimbali ambavyo kiujumla vinaimarisha kinga ya mwili. Kupungua uzito kwa sababu ya kiwango kikubwa cha nyuzi chakula/ Fiber, hizi zitasaidia kushibisha, na hivyo kupunguza tamaa ya kula isiyo rasmi. Msaada wa Kulala. R...
""AHSANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU, KARIBU TENA/ THANK YOU FOR VISITING OUR BLOG, YOU ARE WELCOME""