Skip to main content
""Kwa msaaada zaidi wasiliana nasi kwa namba zifuatazo 0754031039/0655568468 AfyaLishe Tz kwa ajili yako""

COUNSELLING DESK

COUNSELLING DESK
Tumia huduma yetu ya ushauri, na kujadiliana. Kwa matatizo ya kifamilia, kibiashara, kielimu, kiafya, mahusiano na mfumo mzima wa maisha wasiliana nasi kwa 0754031039 au 0655568468

DODOSO LA KUMPOKEA MSAIDIZI WA KAZI ZA NYUMBANI


1. Majina kamili
2. Umri
3. Historia ya familia
4. Historia ya elimu
5. Historia ya Afya
6. Historia ya kazi na kwanini aliacha.
7. Ratiba yake ya siku
8. Kazi anazoweza kufanya
9. Kazi asizoweza kufanya na kwanini.
10. Aina ya vyakula asivyoweza kula na kwanini
11. Tambua Dini yake na imani zake.

*Zingatia*

●Baada ya kumdodosa dada, andika majibu yake na utumie hayo kumpangia majukumu yake na kanuni za kazi hapo kwako.

●Ni muhimu dada kupima afya yake pindi anapoingia kwako.

●Ni muhimu dada kuwa na barua ya utambulisho kutoka kijiji alipotoka iliyosainiwa ns yenye muhuri na saini ya mwenyekiti wake

●Ni muhimu dada kuja na kithibitisho cha wazazi au walezi wake kuridhia kufanya kazi hapo na uwe na mawasiliano nao.

●Ni muhimu kuweka wazi ratiba za likizo

●Ni muhimu kuweka wazi matumizi yatakayokua juu yako na atakayojitegemea

●Ni muhimu kumuandalia ratiba ya kazi itakayomuongoza kwa siku nzima.

●Ikiwezekana binti akaguliwe vitu alivyokuwa navyo anavyofika.

●Msisitize binti kuhusu usafi wa mwili wake na wa mazingira pamoja na chakula wakati anandaa

●Muajiri jitahidi kuishi na binti kwa upendo mpe motisha na kumpongeza anapofanya vizuri na kumuelekeza vizuri pale anapokosea ili ajifunze na si kumkaripia kila mara au hata kumpiga.

Angalizo: Iwapo utamnunulia binti zawadi mf. Nguo fanya kwa kiasi ili azoee, wengi hufurahi kuoitiliza na kutaka kurudi kwao kuringishia nguo zao na hii sio nzuri kwa muajiri

●Binti aelekezwe kupokea wageni na ndugu kwa ukarimu, lakini pia muajiri usiseme siri za familia au kumsema mtu wa familia mbele ya binti.

●kama una watoto waelekeze kujitegemea na kushiriki baadhi ya kazi, usijisahau ukaharibu watoto sababu wanafanyiwa kila kitu.

●Binti asaini mkataba unaoelekeza majukumu yake na kanuni za kazi na malipo yake.

●Binti asiaini kila anapopokea mshahara


```Lengo ni kujenga mipaka,heshima na usalama wa kazi.```

*Resta Dietetics &* *Counselling*
*0754031039*

```Karibu kwenye group letu, ujifunze lishe bora na mambo mengine mengi.```

https://chat.whatsapp.com/BFXj5ZT2p794abU8NAxJ0k

```Bonyeza link hapo juu kujiunga moja kwa moja.```

Comments

NEWS

NEWS
Kula lishe bora kuepuka hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa.

Chagua afya leo.

EXCLUSIVE BREASTFEEDING

EXCLUSIVE BREASTFEEDING
Make sure your child gets breastfed exclussively for the first six months, the child shouod not be fed anything else not even water. This adds up to the child's immunity and increase chencea of proper development.

Popular posts from this blog

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA Tumekua na tamaduni ya kuandaa uji wa lishe ya mtoto bila kufuata kanuni za uandaaji bora. Madhara ya uji usio bora

UANDAAJI MAZIWA YA SOYA UKIWA NYUMBANI

Maziwa ya Soya Aina hii ni maarufu pia, na kwa kuwa yanatokana na mimea, maziwa haya hana cholesterol ( lehemu) - tofauti na maziwa ya kawaida. Maziwa ya Soya pia yana kiwango cha chini cha kalori kuliko maziwa ya ng'ombe, yana kalori takribani 130 kwa kila kikombe. Hakuna lactose  katika maziwa haya, aina ya protini inayoleta sana gesi tumboni, hivyo huyafanya kuwa mbadala muhimu kwa watu ambao wanakabiliwa na ugonjwa wa kushindwa kuvumilia lactose (lactose intolerance) katika mfumo wao wa umeng'enyaji, pamoja na watu wasiotumia bidhaa zitokanazo na wanyama pia (vegeterians) sababu haitoki kwa wanyama.  Soya ni mboga nzuri sana, na maziwa yanayotokana na jamii hii yana utajiri wa potasiamu, protini na kalsiamu ikiwa mtengenezaji atayaimarisha na madini. Pia ni chanzo kikubwa cha vitamini A na vitamini B12, ambayo haipo katika aina nyingine za maziwa. Maziwa ya Soya hutoa kiwango cha juu cha protini, pia ni bora kwa watu ambao wanajaribu kudhibiti uzito wao au kupu...

MORINGA BENEFITS/ FAIDA ZA MLONGE

MLONGE Inaweza kutumika kwa ajili ya upishi na dawa. Mbegu hizi ni chakula ila  zinapaswa kutafunwa, badala ya kuzimeza nzima nzima, pia ni muhimiu zikapikwa au kukaushwa kabla ya kuliwa, badala ya kula mbichi. UMUHIMU KATIKA LISHE Mbegu za Moringa ni chanzo kikubwa cha Madini chuma, Potasiamu, Vitamini A, Vitamini C, Calcium, Amino asidi, na Nyuzi za chakula/Fibers. FAIDA ZAKE KIUNDANI -Huongeza mfumo wa kinga ya mwili. -Hupunguza shinikizo la damu. -Kurahisisha upatikanaji wa usingizi, na -Kuongeza afya ya ngozi, nywele na mifupa. MAELEZO KWA KINA. Huongeza mfumo wa kinga ya mwili. Uchunguzi umegundua kwamba mbegu hizi zina tabia za kinga dhidi ya vimelea na virusi, kutokana na mkusanyiko wao mkubwa wa vitamini C, pamoja na viuasumu mbalimbali ambavyo kiujumla vinaimarisha kinga ya mwili. Kupungua uzito kwa sababu ya kiwango kikubwa cha nyuzi chakula/ Fiber, hizi zitasaidia kushibisha, na hivyo kupunguza tamaa ya kula isiyo rasmi. Msaada wa Kulala. R...
""AHSANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU, KARIBU TENA/ THANK YOU FOR VISITING OUR BLOG, YOU ARE WELCOME""