Skip to main content
""Kwa msaaada zaidi wasiliana nasi kwa namba zifuatazo 0754031039/0655568468 AfyaLishe Tz kwa ajili yako""

COUNSELLING DESK

COUNSELLING DESK
Tumia huduma yetu ya ushauri, na kujadiliana. Kwa matatizo ya kifamilia, kibiashara, kielimu, kiafya, mahusiano na mfumo mzima wa maisha wasiliana nasi kwa 0754031039 au 0655568468

JE UNATUMIA VIGEZO VIPI KUANZA MAHUSIANO MAPYA



Siku hizi tumejisahau sana!!!
Wengi wetu angalau tumepata neema ya kusoma chekechea ama basi hata darasa la kwanza.

Hiki huwa kipindi muhimu kwetu maana unaanza kuingia katika jamii, wale uliowazoea nyumbani sio utakaowakuta huko shule, namaanisha unakutana na watu wasiokuhusu kwa asilimia 100.

Lakini kadri unavyoishi nao unajikuta mnafahamiana kisha mtakutana kwenye michezo kisha kuna kikundi cha watu wawili watatu ambacho utajikuta umeingia bila mpango ama kutambua ila basi tu ndio mmeendana na mnakua marafiki wa karibu (best friends) kuanzia hapo.

Hii ndio stage kubwa ya mwanzo utaanza nahusiano. Ila utakubaliana na mimi pindi utakapohamia level ingine ya kielimu, wale wa nyuma utawasahau kabisa na ni wachache huweza kumaintain urafiki huu hadi utuuzima au hata mawasiliano tu.

Kwanini nimetumia mfano huo?

Hii ni sababu hata na utu uzima huu tumepoteza mahusiano ya wale watu wa muhimu kwetu wanaotuhusu asilimia 100 na kuingia katika kujali mahusiano na watu wasiotuhusu kwa asilimia 100.

Unaweza ukawa hujaelewa bado  ninachojaribu kukwambia.

Jiulize kati ya shosti yako mliokutana group la whatsaap au yule jamaa uliokutana nae katika bar jioni ukipumzika na yule wa karibu yako unaeishi nae nyumba moja yupi unampa nafasi na je ikitokea una tatizo ni nani atakupa nafasi???

Nafkiri unajiuliza na kuna majibu umepata

Ndugu yangu katika maisha Jifunze kumpa kila mtu umuhimu kulingana na umuhimu atakaokupa wewe kipindi upo katika shida ya ndani.

Wanaume wanamuona bar maid ah mchepuko ni wa muhimu zaidi au yule msela wake ni muhimu zaidi kuliko mke wake wa ndani.

Mpaka kipindi mtu anakufa ndio mke wake anajua kua kumbe kuna nyumba iko sehemu flani au kuna kiwanja kipo sehemu fulani. Familia inaingia mafarakano na watoto ndio wanaopata tabu.

Wanawake wengi wamepoteza ndoa zao kwa ujinga wa mashosti wa facebook, whatsapp, instagram na vibarazani, wanatumia experience za marafiki kuhimili au kutatua changamoto katika familia yake na kusahsu kua mume wa shosti ni engineer na wake ni daktari, hawa watu wapo  mazingira tofauti kabisa halafu wote unataka kutumia formula moja kuishi nao!!!, unashangaa kama alikua anarudi saa tatu usiku ndio anarudi asubuhi. Nani wa kumlaumu?

Vijana wengi wamejikuta kwenye mahusiano wasiyoyastahili ya baadae unakua mzigo mzito na huwez kuutua tena maana ukiangalia unaona umepoteza muda, na kwa umri wako sasa hivi unawaza utaanzaje upya.
Nani wa kukaumiwa???

Hakikisha unachagua kwa makini jinsi ya kutumia muda wako katika mahusiano unayokutana nayo.

Sio lazima muwe karibu sana, sio lazima ajue siri zako, wacha Mungu azijue siri zako maana ndipo pekee itabaki kua siri na utapata jawabu la kudumu.

Usiruhusu mahusiano yasiyo na faida yakupotezee muda wako na mahusiano yako yakudumu.

Usiingie katika mahusiano kama mtoto alieanza kindergatten au la kwanza.  Ukashangaa kipindi cha shida wale wa nyumbani wote umewapoteza na yule uliemuona wa karibu yupo busy na watu wanaomuhusu kwa asilimia 100. Katika hatua hii ndio utagundua kwamba sio kila muda kuna second chance!!!


By Resta Dietetics & Counselling
0754031039

```Karibu kwenye group letu, ujifunze lishe bora na mambo mengine mengi.```

https://chat.whatsapp.com/BFXj5ZT2p794abU8NAxJ0k

```Bonyeza link hapo juu kujiunga moja kwa moja.```

Comments

NEWS

NEWS
Kula lishe bora kuepuka hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa.

Chagua afya leo.

EXCLUSIVE BREASTFEEDING

EXCLUSIVE BREASTFEEDING
Make sure your child gets breastfed exclussively for the first six months, the child shouod not be fed anything else not even water. This adds up to the child's immunity and increase chencea of proper development.

Popular posts from this blog

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA Tumekua na tamaduni ya kuandaa uji wa lishe ya mtoto bila kufuata kanuni za uandaaji bora. Madhara ya uji usio bora

UANDAAJI MAZIWA YA SOYA UKIWA NYUMBANI

Maziwa ya Soya Aina hii ni maarufu pia, na kwa kuwa yanatokana na mimea, maziwa haya hana cholesterol ( lehemu) - tofauti na maziwa ya kawaida. Maziwa ya Soya pia yana kiwango cha chini cha kalori kuliko maziwa ya ng'ombe, yana kalori takribani 130 kwa kila kikombe. Hakuna lactose  katika maziwa haya, aina ya protini inayoleta sana gesi tumboni, hivyo huyafanya kuwa mbadala muhimu kwa watu ambao wanakabiliwa na ugonjwa wa kushindwa kuvumilia lactose (lactose intolerance) katika mfumo wao wa umeng'enyaji, pamoja na watu wasiotumia bidhaa zitokanazo na wanyama pia (vegeterians) sababu haitoki kwa wanyama.  Soya ni mboga nzuri sana, na maziwa yanayotokana na jamii hii yana utajiri wa potasiamu, protini na kalsiamu ikiwa mtengenezaji atayaimarisha na madini. Pia ni chanzo kikubwa cha vitamini A na vitamini B12, ambayo haipo katika aina nyingine za maziwa. Maziwa ya Soya hutoa kiwango cha juu cha protini, pia ni bora kwa watu ambao wanajaribu kudhibiti uzito wao au kupu...

MORINGA BENEFITS/ FAIDA ZA MLONGE

MLONGE Inaweza kutumika kwa ajili ya upishi na dawa. Mbegu hizi ni chakula ila  zinapaswa kutafunwa, badala ya kuzimeza nzima nzima, pia ni muhimiu zikapikwa au kukaushwa kabla ya kuliwa, badala ya kula mbichi. UMUHIMU KATIKA LISHE Mbegu za Moringa ni chanzo kikubwa cha Madini chuma, Potasiamu, Vitamini A, Vitamini C, Calcium, Amino asidi, na Nyuzi za chakula/Fibers. FAIDA ZAKE KIUNDANI -Huongeza mfumo wa kinga ya mwili. -Hupunguza shinikizo la damu. -Kurahisisha upatikanaji wa usingizi, na -Kuongeza afya ya ngozi, nywele na mifupa. MAELEZO KWA KINA. Huongeza mfumo wa kinga ya mwili. Uchunguzi umegundua kwamba mbegu hizi zina tabia za kinga dhidi ya vimelea na virusi, kutokana na mkusanyiko wao mkubwa wa vitamini C, pamoja na viuasumu mbalimbali ambavyo kiujumla vinaimarisha kinga ya mwili. Kupungua uzito kwa sababu ya kiwango kikubwa cha nyuzi chakula/ Fiber, hizi zitasaidia kushibisha, na hivyo kupunguza tamaa ya kula isiyo rasmi. Msaada wa Kulala. R...
""AHSANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU, KARIBU TENA/ THANK YOU FOR VISITING OUR BLOG, YOU ARE WELCOME""