Skip to main content
""Kwa msaaada zaidi wasiliana nasi kwa namba zifuatazo 0754031039/0655568468 AfyaLishe Tz kwa ajili yako""

COUNSELLING DESK

COUNSELLING DESK
Tumia huduma yetu ya ushauri, na kujadiliana. Kwa matatizo ya kifamilia, kibiashara, kielimu, kiafya, mahusiano na mfumo mzima wa maisha wasiliana nasi kwa 0754031039 au 0655568468

JE UNATUMIA VIGEZO VIPI KUANZA MAHUSIANO MAPYA



Siku hizi tumejisahau sana!!!
Wengi wetu angalau tumepata neema ya kusoma chekechea ama basi hata darasa la kwanza.

Hiki huwa kipindi muhimu kwetu maana unaanza kuingia katika jamii, wale uliowazoea nyumbani sio utakaowakuta huko shule, namaanisha unakutana na watu wasiokuhusu kwa asilimia 100.

Lakini kadri unavyoishi nao unajikuta mnafahamiana kisha mtakutana kwenye michezo kisha kuna kikundi cha watu wawili watatu ambacho utajikuta umeingia bila mpango ama kutambua ila basi tu ndio mmeendana na mnakua marafiki wa karibu (best friends) kuanzia hapo.

Hii ndio stage kubwa ya mwanzo utaanza nahusiano. Ila utakubaliana na mimi pindi utakapohamia level ingine ya kielimu, wale wa nyuma utawasahau kabisa na ni wachache huweza kumaintain urafiki huu hadi utuuzima au hata mawasiliano tu.

Kwanini nimetumia mfano huo?

Hii ni sababu hata na utu uzima huu tumepoteza mahusiano ya wale watu wa muhimu kwetu wanaotuhusu asilimia 100 na kuingia katika kujali mahusiano na watu wasiotuhusu kwa asilimia 100.

Unaweza ukawa hujaelewa bado  ninachojaribu kukwambia.

Jiulize kati ya shosti yako mliokutana group la whatsaap au yule jamaa uliokutana nae katika bar jioni ukipumzika na yule wa karibu yako unaeishi nae nyumba moja yupi unampa nafasi na je ikitokea una tatizo ni nani atakupa nafasi???

Nafkiri unajiuliza na kuna majibu umepata

Ndugu yangu katika maisha Jifunze kumpa kila mtu umuhimu kulingana na umuhimu atakaokupa wewe kipindi upo katika shida ya ndani.

Wanaume wanamuona bar maid ah mchepuko ni wa muhimu zaidi au yule msela wake ni muhimu zaidi kuliko mke wake wa ndani.

Mpaka kipindi mtu anakufa ndio mke wake anajua kua kumbe kuna nyumba iko sehemu flani au kuna kiwanja kipo sehemu fulani. Familia inaingia mafarakano na watoto ndio wanaopata tabu.

Wanawake wengi wamepoteza ndoa zao kwa ujinga wa mashosti wa facebook, whatsapp, instagram na vibarazani, wanatumia experience za marafiki kuhimili au kutatua changamoto katika familia yake na kusahsu kua mume wa shosti ni engineer na wake ni daktari, hawa watu wapo  mazingira tofauti kabisa halafu wote unataka kutumia formula moja kuishi nao!!!, unashangaa kama alikua anarudi saa tatu usiku ndio anarudi asubuhi. Nani wa kumlaumu?

Vijana wengi wamejikuta kwenye mahusiano wasiyoyastahili ya baadae unakua mzigo mzito na huwez kuutua tena maana ukiangalia unaona umepoteza muda, na kwa umri wako sasa hivi unawaza utaanzaje upya.
Nani wa kukaumiwa???

Hakikisha unachagua kwa makini jinsi ya kutumia muda wako katika mahusiano unayokutana nayo.

Sio lazima muwe karibu sana, sio lazima ajue siri zako, wacha Mungu azijue siri zako maana ndipo pekee itabaki kua siri na utapata jawabu la kudumu.

Usiruhusu mahusiano yasiyo na faida yakupotezee muda wako na mahusiano yako yakudumu.

Usiingie katika mahusiano kama mtoto alieanza kindergatten au la kwanza.  Ukashangaa kipindi cha shida wale wa nyumbani wote umewapoteza na yule uliemuona wa karibu yupo busy na watu wanaomuhusu kwa asilimia 100. Katika hatua hii ndio utagundua kwamba sio kila muda kuna second chance!!!


By Resta Dietetics & Counselling
0754031039

```Karibu kwenye group letu, ujifunze lishe bora na mambo mengine mengi.```

https://chat.whatsapp.com/BFXj5ZT2p794abU8NAxJ0k

```Bonyeza link hapo juu kujiunga moja kwa moja.```

Comments

NEWS

NEWS
Kula lishe bora kuepuka hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa.

Chagua afya leo.

EXCLUSIVE BREASTFEEDING

EXCLUSIVE BREASTFEEDING
Make sure your child gets breastfed exclussively for the first six months, the child shouod not be fed anything else not even water. This adds up to the child's immunity and increase chencea of proper development.

Popular posts from this blog

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA Tumekua na tamaduni ya kuandaa uji wa lishe ya mtoto bila kufuata kanuni za uandaaji bora. Madhara ya uji usio bora

KANUNI BORA ZA KUMUANZISHIA MTOTO CHAKULA AFIKAPO MIEZI SITA

KANUNI BORA ZA KUMUANZISHIA MTOTO CHAKULA AFIKAPO MIEZI SITA 🏮 Kwanini nianze kumpa mtoto wa miezi 6 chakula kingine? 🍲Mtoto wa miezi sita ameanza kuwa na mahitaji ya virutubishi  kwa wingi zaidi ya anavyopata kutoka kwenye maziwa ya mama.

ONGEZA UWEZO WAKO WA KUMNYONYESHA MTOTO

ONGEZA UWEZO WAKO WA KUMNYONYESHA MTOTO Mtoto anyonye maziwa ya mama tu hadi ayakapotimiza Miezi sita. Utakua umemuepushia magonjwa na hatari zingine nyingi tu. Kama mama hana maziwa ya kutosha mtoto pia anaweza kupewa formula milk ila ni pale tu mama akiwa maefariki au akiwa na tatizo kama hilo la maziwa kuto tosha. Lakini ni muhimu mama kukazana kuhakikisha maziwa yanatosha ili mtoto awe katika hali salama na afya zaidi. Fahamu vitu vifuatavyo vimesaidia wengine 🍵Maziwa ya mama yametengenezwa na vtu vi3 vya muhimu *maji ambayo ndio mengi *Protein and *Fats 🍵 ni muhimu sana kufahamu kwamba  kutoka kwa  Maziwa kunahitaji activity ya hormones/ homoni ziwe stimulated, na kinachostimulate ni mtoto kunyonya au kuvuta chuchu Hivyo mtoto anavovuta au kunyonya chuchu ya mama yake ndivo hormones za kutengeneza  maziwa zinavozalishwa zaidi, hivyo kuleta matokeo chanya katika unyonyeshaji. Mama asikate tamaa kumueka mtoto kwenye chuchu hata kama maziwa hayatoki auni macha
""AHSANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU, KARIBU TENA/ THANK YOU FOR VISITING OUR BLOG, YOU ARE WELCOME""