Skip to main content
""Kwa msaaada zaidi wasiliana nasi kwa namba zifuatazo 0754031039/0655568468 AfyaLishe Tz kwa ajili yako""

COUNSELLING DESK

COUNSELLING DESK
Tumia huduma yetu ya ushauri, na kujadiliana. Kwa matatizo ya kifamilia, kibiashara, kielimu, kiafya, mahusiano na mfumo mzima wa maisha wasiliana nasi kwa 0754031039 au 0655568468

SAYANSI NYUMA YA DETOX NA KUPUNGUZA UNENE, UZITO AU VITAMBI


MAKALA YA 102

http://afyalishetz.blogspot.com/2019/07/sayansi-nyuma-ya-detox-na-kupunguza.html

N:B Asilimia 60  ya uzito ulionao ni maji, hivyo kadri unavyopoteza maji ndivyo unapoteza uzito.

Mf: Mtu mwenye kilo kg100 akifanikiwa kupoteza lita 10 za maji mwilini mwake, atakua amefanikiwa kupunguza kilo kg14 za uzito wake.

Katika dunia ya leo kila mtu anahitaji kuwa na mwili unaovutia na kupendeza. Kwa bahati mbaya wengi tunatamani hili bila ya kulifanyia kazi.

Kutokana na tamaa hii tuliyonayo basi tumeibua ushawishi kwa wajasiriamali wengi kuanza biashara ya uuzaji wa detox tea
(chai za kusafisha na kupunguza mwili)

Nimeandika ili kwa wale tusio fahamu tujifunze kitu.

```Tuanzie hapa
Nini maana ya detox?
Kwa lugha ya wenzetu Toxin ni sumu, hivyo Detox ni kitendo cha kuiondoa hiyo sumu.

Sasa kwa vile hapa naongelea zaidi mwili, naweza nikasema Detox ni kuondoa sumu mwilini.

Vinywaji vya Detox huwa na *Antioxidants*, kwa lugha rahisi tunaweza kusema ni *Viua sumu*.

Viungo kama vitunguu swaumu, mchai chai, karafuu, hata matunda pia huwa na hivi vitu viitwavyo viua sumu, ambavyo hutumika kusafisha mwili na kuondoa sumu,  kwa njia ya kurahisisha umeng'enyaji wa chakula hivyo mtu anaweza kupata choo kizuri kila siku ambayo ni njia nzuri ya kuzuia sumu zisifyonzwe mwilini na kutoka kwa njia ya kupata choo.

Kama umenielewa naweza nikakwambia kwamba, katika mauzo ya hizi detox tea, wauzaji watakwambia:

'' Mteja wangu hii detox usipokula vizur na kufanya mazoezi hautapata matokeo mazuri, hivyo kua makini''

 Hii humfanya mteja alietumia pesa yake nyingi, kujitahidi kula vizur na kufanya zoezi pamoja na kutumia Detox yake huku akiamini atapungua na kweli ndani ya wiki ama wiki mbili mtu huanza kuona matokeo chanya.

Pia wauzaji wengine huenda zaidi na kusema kwamba:

 ''ukiacha kutumia hii detox utarudia tena unene na kitambi kitarudi kama kilivyokua''

```Jiulize swali.........```

Je kilichompunguza huyu mtu ni detox tea au kula vizur na mazoezi?

```JE KUNA MADHARA YOYOTE YA KUTUMIA DETOX```

Detox nyingi huwa hazina kemikali mbaya, huwa ni bidhaa mbali mbali za asili mfano, mchai chai, karafuu, n.k ambavyo huwa havina madhara.

▪Lakini ili kuongeza ufanisi wake wa kufanya kazi kwa haraka kuna kemikali huwa zinaongezwa.

Ndio pale utasikia muuzaji anakwambia:

 "Detox hii ukitumia hata ukila vipi ni lazima tu utapungua maana ina flush kila kitu"

▪Mara nyingi Detox huweza kuwa na kemikali za kukufanya kuwa active au mchangamfu na mwenye nguvu kwa muda bila kusikia njaa.

▪Pia inaweza kukufanya ukaharisha sana sababu ya kuwa na laxatives
(madawa yanayotumika kutibu constipation).
Na hii hupelekea kupunguza mwili kwa kupoteza maji mwilini.

Kwa mantiki iliyoelezwa mwanzoni kabisa mwa nakala hii, Matumizi ya Detox hupunguza zaidi maji (water weight) na sio sumu kama inavotangazwa.
Kadri unavyopoteza maji ndivyo unavyopoteza uzito

▪Kutokana na hii,  kuharisha kupitiliza kunaweza pia kusababisha(electrolyte imbalance), kupotezwa kwa madini mengi ya chumvi chumvi ( sodium chloride) ambazo zinazotumika kusawazisha maji ya mwilini na kufanikisha baadhi ya shughuli za figo.

▪Pia utendaji wa misuli huweza kufifishwa, na hii ni hatari kwasababu inaweza kupooza ufanisi wa misuli ya kawaida na ukawa kama huna control na movement za misuli yako lakini pia misuli ya kwenye moyo na kusababisha mapigo ya moyo kutokua sawa.

▪Madawa haya pia  yakitumika muda mrefu yanaweza kuathiri ( Bowel movements) utendaji wa utumbo  katika kumeng'enya chakula na kusababisha uwe unategemea hizo laxatives ili kupata choo vizur na si kwa njia ya kawaida tena yaani bila matumizi ya madawa.

▪Pia unaweza ukapata matatizo ya kichefu chefu, tumbo kujaa gesi na maumivu ya tumbo.

▪Ukosefu wa usingizi tulivu kwasababu baadhi ya Detox huwa na caffein na ikizidi kiwango kwa siku huweza sababisha ukosefu wa usingizi mtulivu.

▪Pia kama upo kwenye dozi tofauti baadhi ya detox zinaweza kuathiri utendaji sahihi wa dozi hizo, maana zinaweza kutoka mwilini kwa njia ya mkojo au kuharisha kabla hata hazijafanya kazi yake mwilini.

USHAURI WETU

Matumizi ya Detox yawe kwa kiasi, pia hakikisha Detox unazotumia zimeruhusiwa na kupitishwa kwa matumizi na TMDA/ TBS au shirika zingine kwa nchi jirani.

Njia sahihi ya kupata mwili bora ni kwa kuzingatia ulaji sahihi ( healthy weight loss Diets) na ufanyaji wa mazoezi.

```Karibu kwa ushauri zaidi kuhusu lishe bora za watoto na rika zote, diet za kudhibiti uzito, kisukari, presha n.k .```

_Imeandikwa na ;_
_Sylvia Senkoro_

Resta Dietetics & Counselling
0754031039

Cc: CHOICELINE Co. Ltd

Comments

NEWS

NEWS
Kula lishe bora kuepuka hatari ya kupata magonjwa yasiyoambukizwa.

Chagua afya leo.

EXCLUSIVE BREASTFEEDING

EXCLUSIVE BREASTFEEDING
Make sure your child gets breastfed exclussively for the first six months, the child shouod not be fed anything else not even water. This adds up to the child's immunity and increase chencea of proper development.

Popular posts from this blog

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA

UANDAAJI WA LISHE YA UJI UNAOTAKIWA KWA MTOTO MIEZI SITA NA KUENDELEA Tumekua na tamaduni ya kuandaa uji wa lishe ya mtoto bila kufuata kanuni za uandaaji bora. Madhara ya uji usio bora

KANUNI BORA ZA KUMUANZISHIA MTOTO CHAKULA AFIKAPO MIEZI SITA

KANUNI BORA ZA KUMUANZISHIA MTOTO CHAKULA AFIKAPO MIEZI SITA 🏮 Kwanini nianze kumpa mtoto wa miezi 6 chakula kingine? 🍲Mtoto wa miezi sita ameanza kuwa na mahitaji ya virutubishi  kwa wingi zaidi ya anavyopata kutoka kwenye maziwa ya mama.

ONGEZA UWEZO WAKO WA KUMNYONYESHA MTOTO

ONGEZA UWEZO WAKO WA KUMNYONYESHA MTOTO Mtoto anyonye maziwa ya mama tu hadi ayakapotimiza Miezi sita. Utakua umemuepushia magonjwa na hatari zingine nyingi tu. Kama mama hana maziwa ya kutosha mtoto pia anaweza kupewa formula milk ila ni pale tu mama akiwa maefariki au akiwa na tatizo kama hilo la maziwa kuto tosha. Lakini ni muhimu mama kukazana kuhakikisha maziwa yanatosha ili mtoto awe katika hali salama na afya zaidi. Fahamu vitu vifuatavyo vimesaidia wengine 🍵Maziwa ya mama yametengenezwa na vtu vi3 vya muhimu *maji ambayo ndio mengi *Protein and *Fats 🍵 ni muhimu sana kufahamu kwamba  kutoka kwa  Maziwa kunahitaji activity ya hormones/ homoni ziwe stimulated, na kinachostimulate ni mtoto kunyonya au kuvuta chuchu Hivyo mtoto anavovuta au kunyonya chuchu ya mama yake ndivo hormones za kutengeneza  maziwa zinavozalishwa zaidi, hivyo kuleta matokeo chanya katika unyonyeshaji. Mama asikate tamaa kumueka mtoto kwenye chuchu hata kama maziwa hayatoki auni macha
""AHSANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU, KARIBU TENA/ THANK YOU FOR VISITING OUR BLOG, YOU ARE WELCOME""